Search This Blog

Tuesday, April 20, 2021

Watu 12 wapoteza maisha kwenye mlipuko wa tanki la mafuta nchini Nigeria

Kulingana na ripoti za awali, watu 12 walipoteza maisha katika mlipuko uliotokea baada ya ajali ya kupinduka kwa tanki la mafuta kutokea katika jimbo la Benue nchini Nigeria.

Mratibu wa Jimbo la Benue wa Shirika la Kitaifa la Usalama wa Barabarani (FRSC) Yakubu Muhammed, aliliambia gazeti la eneo hilo kwamba mlipuko ulitokea baada ya tanki la mafuta kupinduka kwenye barabara ya jimbo la Oshigbudu-Obagaji.

Muhammed alisema kuwa kulingana na taarifa za awali juu ya mlipuko huo, watu 12, wakiwemo wanawake 3 na mtoto, walipoteza maisha na watu wengine wengi walijeruhiwa.

Akielezea kuwa majeruhi wengine wako katika hali mbaya, Muhammed alielezea wasiwasi wake juu ya ongezeko la idadi ya vifo.

Muhammed pia alisema kuwa nyumba na maduka ya maeneo ya jirani pia yailiharibiwa kutokana na mlipuko huo.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...