Viongozi wa kigeni walitoa ujumbe wa kusherehekea mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Katika ujumbe wa Rais wa Marekani (USA) Joe Biden, alisherehekea mwezi wa Ramadhan na ulimwengu wa Kiislamu na akaangazia uhalifu wa chuki dhidi ya Waislamu nchini humo.
Biden aliweka msisitizo kwa kutumia maneno haya: "Waislamu bado ni walengwa wa uonevu, ukatili na uhalifu wa chuki." Biden alisisitiza kuwa mambo haya hayawezi kukubalika.
Akielezea kuwa Waislamu Wamarekani wameitajirisha nchi hiyo tangu siku ya kwanza ya uanzilishi wake, Biden alisema,
"Waislamu wamekuwa safu za mbele kwenye mapambano yetu dhidi ya Covid-19, wakichukuwa jukumu kubwa katika ukuzaji wa chanjo (dhidi ya corona) na kushughulika kama wafanyikazi wa huduma ya afya."
Biden alisema kuwa mwaka huu maadhimisho ya Ikulu yatafanyika katika mazingira halisi na kwamba wanatarajia kufanya sherehe ya jadi ya likizo ya Ikulu mwaka ujao uso kwa uso na mkewe Jill.
Katika ujumbe wa Waziri Mkuu wa Ujerumani Angela Merkel, pia alitaka Waislamu wote wawe na "Ramadhan ya amani".
Akisisitiza kuwa Ramadhan ni mwezi wa mshikamano, Merkel alisema kuwa ni muhimu kuwa wavumilivu katika kipindi hiki kigumu kwa sababu ya janga.
Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson, ambaye alisherehekea mwezi wa Ramadhan kwa ulimwengu wa Kiislamu pia alichapisha ujumbe kwenye akaunti yake ya mtandao wa kijamii, na kusema kwamba Ramadhan itakuwa tofauti mwaka huu kwa sababu ya janga.
Johnson alisema,
"Natumai mwezi huu wa kufunga, sala na hisani utaleta amani nyingi kwa Waislamu wote."

No comments:
Post a Comment