Search This Blog

Saturday, April 17, 2021

Kiongozi wa kijeshi wa Myanmar kuhudhuria mkutano wa ASEAN


Kiongozi wa kijeshi nchini Myanmar, Min Aung Hlaing atahudhuria mkutano wa kilele wa viongozi wa Umoja wa Mataifa ya Kusini/mashariki mwa Asia, (ASEAN) ambao unatarajiwa kufanyika Aprili 24 nchini Indonesia. 

Taarifa hizo ni kwa mujibu wa wizara ya mambo ya nje ya Thaland.Viongozi kadhaa ya mataifa 10 ya ASEAN, ambapo pia Myanmar ni mwanachama, wamethibitisha mahudhirio yao katika mkutano huo utakaofanyika Jakarta, akiwemo kiongozi huyo wa kijeshi wa Myanmar.

Mataifa jirani na Myanmar yamekuwa yakipigia chapuo mazungumzo ya amani kati ya pande zinazohasimiana nchini humo kwa lengo la kuyafikisha kikomo machafuko ambayo yalitokea baada ya mapinduzi ya kijeshi ya Feburuari Mosi.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...