Search This Blog

Tuesday, April 13, 2021

Iran yasema shambulio limeuharibu vibaya mtambo wake wa nyuklia


Maelfu ya mashine zinazotumika kurutubisha nyenzo za nyuklia zimeharibiwa katika shambulio lililotokea kwenye mtambo muhimu, Jumapili, maafisa wa Iran wamesema.

Alireza Zakani, mkuu wa kituo cha Utafiti cha Bunge la Iran, amesema shambulio hilo "limeondoa" uwezo wa Iran wa kutekeleza mchakato huo.

Shambulizi hilo limetokea katika mtambo ulio mita 50 chini ardhi, afisa mwingine amesema.

Iran imelaumu Israel kwa kile ilichokiita kitendo cha "ugaidi wa kinyuklia".

Israel bado haijathibitisha wala kukanusha madai hayo, lakini kituo cha redio cha Israel kinachomilikiwa na serikali kimenukuu vyanzo vya kijasusi vikisema ilikuwa operesheni ya kimtandao ya Masaad.

Iran imesema itabadilisha mashine zilizoathirika - zile zinazotumika kuimarisha au kurutubisha, kemikali ya urani inayotumika katika uzalishaji wa nishati ya nyuklia au mabomu ya nyuklia - na hata kuweka mashine za kisasa zaidi.

Pia, Jumatano imetangaza kuwa itaongeza kiwango chake cha urutubishaji - kutoka asilimia 20 hadi 60. Kiwango hicho kimekatazwa chini ya mkataba wa makubaliano ya nyuklia ya mwaka 2015, huku asilimia 60 ikiwa karibu sana na asilimia 90 inayohitajika kutengeneza silaha za nyuklia.

Wakati huo huo, vyombo vya habari vya Israel na Uarabuni vimesema kuwa meli inayomilikiwa na Israel imeharibiwa katika shambulizi lililotokea pwani ya Milki za Kiarabu.

Maafisa ambao hawakutajwa wamenukuliwa na kituo cha televisheni cha Israel Channel 12, wamelaumu Iran kwa shambulio lililotokea katika meli ya Hyperion Ray. Ikiwa itathibitishwa, hilo litakuwa shambulizi la hivi karibuni katika mfululizo wa mashambulizi ya kulipizana kisasi kati ya meli za Israel na Iran.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...