Makamu wa Rais Dk Philip Mpango amesema fedha ambazo zilikuwa zitumike kwaajili ya kuadhimisha sikukuu ya muungano zimegawanywa katika pande zote mbili kwaajili ya miradi ya maendeleo.
Dk Mpango ameyasema hayo leo Jumatatu Aprili 25, kwenye kongamano la Muungano linalofanyika jijini Dodoma.
Amesema kwa busara za Rais Samia Suluhu amefanya uwamuzi mwaka huu kuadhimisha sikuu ya muungano kwa kufanya kongamano na fedha ambazo zilikuwa zitumike zigawanywe kwenye pande zote mbili za muungano na kila upande utaamua namna ya kuzitumia kwaajili ya shughuli za maendeleo.
"Kwa busara ya mamayetu baada ya kufanya uwamuzi kwamba mwaka huu tuadhimishe muungano wetu kwa kufanya kongamano ameagiza fedha ambazo zilikuwa zitumike kwaajili ya sherehe mwaka huu zitagawanywa kwenda pande zote mbili za muungano na kila upande utaamua namna ya kutumia hizo fedha kwaajili ya miradi ya maendeleo," amesema Dk Mpango

No comments:
Post a Comment