Beijing sasa ni makao ya mabilionea wengi zaidi kuliko miji mingine yoyote duniani, kwa mujibu wa wa orodha ya hivi punde ya Forbe ya watu tajiri.
Mji huo mkuu wa China uliongeza mabilionea 33 mwaka uliopita sasa una mabilionea 100, lilisema gazeti hilo la biashara.
Uliushi kwa karibu mji wa New York, ulio na mabilionea 99 na ambao umekuwa ukiongoza orodhaa hiyo kwa miaka saba mtawalio.
Juhudi za haraka za China kudhibiti ugonjwa wa Covid-19, kupanda ngazi kwa mashirika yake ya kiteknolojia na masoko ya hisa kuliisaidia kupata nafasi hiyo ya kwanza.
Ingawa Beijing sasa ina mabilionea zaidi ya Big Apple, thamani jumla ya mabilionea wa Jiji la New York walisalia kuwa dola bilioni 80 sawa na(Pauni bilioni 58) za Marekani ambayo ni ya juu zaidi kuliko ile ya wenzao wa Beijing.
Mkazi tajiri zaidi wa wa Beijing ni Zhang Yiming, mwanzilishi wa programu tumishi ya kushirikisha video -TikTok na Afisa Mkuu Mtendaji wa kampuni mama ya ByteDance. Thamani ya utajiri wake iliongezek amara mbili hadi dola bilioni 35.6.
Tofauti na mwenzake, mkazi tajiri zaidi wa New York, Meya wa zamani wa Michael Bloomberg, aliye na utajiri wa thamani ya dola bilioni 59.
Mchango wa biashara ya mtandaoni China
China na Marekani zimeshuhudia kukua na kuimarika kwa kampuni zao teknolojiawakati wa janga la corona kwani watu zaidi walianza kununua bidhaa mitandaoni na kutafuta vyanzo vya burudani.
Hali hii ilichangi aukuaji wa mali binafsi ya wamiliki na wenye hisa wa kampuni hizo kubwa za teknolojia.

No comments:
Post a Comment