Search This Blog

Saturday, April 17, 2021

Antony Blinken azungumzia matarajio yake kuhusu hali ya Afghanistan baada ya wanajeshi kuondolewa


Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken alisema kuwa hakutakuwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe tena wakati majeshi ya kigeni yatakapoondoka Afghanistan.

Kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika Afghanistan wakati wa ziara yake, Blinken alisema kuwa wananchi wa Afghanistan hawataki tena vita na kila mtu anataka amani.

Akisisitiza kuwa wataendelea kusaidia vikosi vya serikali ya Afghanistan, Blinken alisema kwamba Taliban inapaswa kutambua kwamba kuachana na michakato ya kisiasa ya kutatua mizozo sio sahihi na haiwezi kuleta suluhisho endelevu.

Blinken alibainisha kuwa baada ya wanajeshi wa Marekani kujiondoa nchini, msaada wao kwa Afghanistan utaendelea.

Akiashiria kwamba baada ya vikosi vya kigeni kuondoka nchini humo hakutakuwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe kama katika miaka ya 1990, Blinken alisisitiza kwamba hakuna mtu anayepaswa kuwa na wasiwasi juu ya suala hili.

Punguza aliongezea kusema,

"Kama Taliban watajaribu kushambulia wanajeshi wetu tena, jibu letu litakuwa zito sana."



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...