Search This Blog

Sunday, April 11, 2021

Ajali katika taasisi ya nyuklia Iran

 


Msemaji wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran Behruz Kemalvendi, aliripoti kuwa ajali ilitokea katika mtandao wa usambazaji umeme kwenye Kiwanda cha Nyuklia cha Natanz huko Isfahan.


Kemalvendi alisema kuwa hakuna mtu aliyejeruhiwa wala hakukuwa na uchafuzi wa mazingira, na kwamba uchunguzi kuhusu chanzo cha tukio hilo unaendelea.


Mnamo Julai 2020, kulikuwa na mkasa wa moto uliozuka katika Kituo cha Nyuklia cha Natanz huko Isfahan, Iran, na madai yalitolewa kwamba lilikuwa ni shambulizi la Israel.


Mlolongo wa centrifuge wa IR6, ulio na vitengo 146 ambavyo vitatoa urani mara 10 zaidi ikilinganishwa na centrifuges zilizopita, ulianza kutumika kwa agizo la Rais Hassan Rouhani hapo jana katika kituo hicho.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...