Waziri Mkuu wa Hungary Viktor Orban amechomwa Chanjo ya Sinopharm, iliyotengenezwa na China , dhidi ya virusi vya corona (Covid-19).
Orban amesema katika taarifa kwamba ilikuwa zamu ya maafisa wa serikali kupewa chanjo hizo na kwamba amechomwa wa kwanza yeye.
Akielezea kwamba alijisikia vizuri sana baada ya chanjo, Orban amesisitiza umuhimu wa chanjo katika wimbi la tatu la corona nchini humo.

No comments:
Post a Comment