Search This Blog

Monday, March 1, 2021

Biden kutoa tamko kuhusu Saudi Arabia leo


Rais wa Marekani Joe Biden amesema leo Jumatatu, Machi 1, Serikali yake itatoa tamko juu ya Saudi Arabia kufuatia ripoti ya kijasusi ya Marekani kusema kuwa mrithi wa kiti cha Ufalme wa taifa hilo, Mohammed Bin Salman aliamuru mauaji ya muandishi habari Jamal Khashoggi.

Utawala wa Biden umekosolewa hasa katika ripoti ya gazeti la Washington Post iliyosema Biden angeonesha nguvu zake kwa Salman ambaye hakuwekewa vikwazo vya aina yoyote licha ya kutajwa kuhusika na mauaji ya Khashoggi.

Biden amesema atatangaza leo Jumatatu hatua watakayochukua kwa Saudi Arabia.

Jamal Khashoggi aliyekuwa uhamishoni Marekani akiandika ripoti zinazomkosoa, Mohammed Salman na Serikali ya Saudi Arabia, aliuwawa Oktoba 2, 2018, katika Ubalozi wa Saudi Arabia mjini Istanbul, Uturuki.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...