Search This Blog

Monday, February 8, 2021

Waziri wa zamani wa Marekani George P. Shultz afariki dunia akiwa na miaka 100


George P. Shultz, ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje kwa zaidi ya miaka 6 chini ya utawala wa Rais wa zamani wa Marekani Ronald Reagan, ameaga dunia.

Katika taarifa iliyotolewa na Taasisi ya Hoover ya Chuo Kikuu cha Stanford, ambapo George P. Shultz alifanya kazi kwa miaka 30, ilielezwa kuwa Waziri huyo wa zamani amefariki akiwa na umri wa miaka 100 nyumbani kwake California.

Shultz, ambaye anachukuliwa kuwa mmoja wa waamuzi wakuu wa kidiplomasia wa Vita vya Baridi viliyotokea kati ya Umoja wa Kisovyeti na Marekani chini ya utawala wa Reagan, pia alikuwa Waziri wa Hazina na Kazi wakati wa rais Richard Nixon.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...