Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu atatekeleza ziara ya Falme za Kiarabu (UAE) tarehe 9 Februari.
Taarifa za vyombo vya habari vya ndani ya nchi ziliarifu kwamba ziara ya Netanyahu kwa UAE itatekelezwa kwa masaa machache.
Taarifa zaidi zimebaini kuwa Netanyahu atakutana na Mkuu wa Utawala wa UAE Mohammed bin Zared ndani ya wigo wa ziara hiyo.
Ilielezwa kuwa ziara ya Netanyahu itafupishwa kutokana na ongezeko la idadi kubwa ya maambukizi ya virusi vya corona kila siku nchini Israeli na majadiliano yaliyopo juu ya kupanua kanuni za karantini.
Netanyahu alipanga kutembelea UAE mara mbili, mnamo Desemba 2020 na mwezi uliopita, lakini ziara hizi zilicheleweshwa kwa sababu tofauti.
Katika ratiba ya mwezi uliopita, Netanyahu alitarajiwa kusafiri UAE kwanza na kisha Bahrain katika ziara yake ya siku 3.
UAE ilifikia makubaliano ya kuhalalisha uhusiano na Israel mnamo Agosti 13, na Bahrain mnamo Septemba 11.
Israel ilitia saini makubaliano na UAE na Bahrain kuhalalisha uhusiano katika hafla iliyofanyika Septemba 15 kwenye Ikulu ya White House nchini Marekani.

No comments:
Post a Comment