Rais wa Ukraine Vladimir Zelenskiy ametangaza kuachiliwa huru kwa mabaharia 6 wa Ukraine waliokuwa wametekwa nyara na maharamia katika pwani ya Nigeria.
Zelenskiy alichapisha ujumbe kwenye mtando wa kijamii wa Instagram na kutambua msaada na mchango mkubwa uliotolewa na wanadiplomasia wa Ukraine katika suala la kuachiliwa huru kwa mabaharia hao.
Meli ya Stevia iliyokuwa na mabaharia 6 wa Ukraine ilivamiwa katika pwani ya Nigeria mwezi mmoja na nusu uliopita. Zelenskiy alisema,
"Raia wetu wapo salama na tunasubiria warudi nchini hivi karibuni."
Maharamia walivamia meli ya Stevia tarehe 16 Desemba 2020 katika pwani ya Nigeria na kuwateka nyara wahudumu 8 wakiwemo mabaharia 6 wa Ukraine.

No comments:
Post a Comment