Search This Blog

Monday, February 15, 2021

Rais Joe Biden kuhudhuria mkutano wa viongozi wa G7 utakaofanyika Februari 19


Rais wa Marekani Joe Biden atahudhuria mkutano wa viongozi wa G7 utakaofanyika siku ya Ijumaa tarehe 19 Februari.

Katika taarifa iliyotolewa na Ikulu ya White House, iliarifiwa kuwa katika mkutano wa viongozi wa G7 ambao utafanyika kwa mara ya kwanza tangu Aprili mwaka jana, Joe Biden atajadili mapambano dhidi ya janga la corona (Covid-19) na ujenzi wa uchumi wa ulimwengu mzima kwa ujumla.

Taarifa zaidi zilieleza kuwa Biden atazingatia ushirikiano katika uanzilishi wa fedha za kiafya dhidi ya tishio la magonjwa ya kuambukiza yanayotokea na uzalishaji, usambazaji na upatikanaji wa chanjo ya Covid-19 kwenye mkutano huo, na ilibainika kuwa matatizo ya kiuchumi yanayosababishwa na China na mgogoro wa hali ya hewa duniani pia zitakuwa kwenye ajenda.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...