Search This Blog

Tuesday, February 23, 2021

Ofisi ya Rais DRC yajiunga na uchunguzi wa mauaji ya balozi wa Italia


Maafisa kutoka ofisi ya rai nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wanatarajiwa kupelekwa mjini Goma kusaidia katika uchunguzi wa mauaji ya balozi wa Italia nchini humo.

Maafisa hao wataondoka leo kuelekea Goma na watakuwa wakiwasilisha ripoti kwa za mara kwa mara kwa rais.

"Mjumbe wa rais wa DRC atazuru [Italia] Jumanne ya leo Februari 23 kuwasilisha barua ya kibinafsi kwa rais wa baraza la Italia," Kulingana na ripoti kutoka kwa idara ya Idara ya habari ya rais.

Katika ujumbe uliyochapishwa katika mtandao wa Twitter, Rais Félix Tshisekedi alisema alisikitishwana taarifa za kufuatia kuuawa kwa mwanadiplomasia wa Italia, Luca Attanasio.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...