Search This Blog

Sunday, February 7, 2021

Misri ipo tayari kukutana na serikali mpya ya Libya


Rais wa Misri Abdulfattah al-Sisi amesema kuwa wako tayari kukutana na serikali mpya itakayoanzishwa nchini Libya.

Katika mahojiano yaliyofanyika kwa njia ya simu na mtangazaji maarufu Amr Edib kwenye idhaa ya "MBC Masr" ya Misri, Sisi alisema kuwa wako tayari kukutana na serikali mpya ya Libya iliyoundwa kwa idhini ya Bunge la Tobruk, ambayo ilichaguliwa na Umoja wa Mataifa (UN) kwenye Mkutano wa Majadiliano ya Kisiasa wa Libya huko Geneva.

Akielezea uchaguzi wa mamlaka kuu nchini Libya kama "hatua inayofaa", Sisi alisema kuwa hali ya nchi hiyo inazidi kuimarika.

Utawala wa Misri ulimpongeza Abdulhamid Dibeybe aliyechaguliwa kama waziri mkuu na  kumtakia mafanikio kwa serikali mpya.

Ahmed al-Mismari ambaye ni msemaji rasmi wa wanamgambo wa vikosi  haramu mashariki mwa nchi, pia alipongeza matokeo ya uchaguzi katika taarifa ya video aliyorekodi hapo jana. Inaripotiwa kuwa taarifa ya Mismari ilidhihirisha vyema nchini Libya.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...