Search This Blog

Monday, February 1, 2021

Mapinduzi Myanmar: Marekani yatishia kuiwekea nchi hiyo vikwazo kwa kuzuiliwa kwa Aung San Suu Kyi

 


Rais wa Marekani Joe Biden ametishia kuirejeshea Myanmar vikwazo baada ya jeshi kupindua serikali.

Jeshi la Myanmar lilimkamata Aung San Suu Kyi na viongozi wengine wa kisiasa wakiwashutumu kwa udanganyifu katika uchaguzi wa hivi karibuni ambao Suu Kyi alipata ushindi mkubwa.

Katika taarifa, Bwana Biden amesema "nguvu isiwahi kutumika kubadilisha maamuzi ya watu au kufuta matokeo ya uchaguzi uliofanyika kwa njia ya halali".

Umoja wa Mataifa na Uingereza pia zimeshutumu mapinduzi hayo.

Marekani ilikuwa imeiondolea nchi hiyo vikwazo zaidi ya muongo mmoja uliopita wakati ambapo Myanmar ilionesha kufuata demokrasia.

Bwana Biden amesema hatua hiyo itapitiwa tena kwa haraka na kuongeza: "Marekani itaunga mkono demokrasia kila itakapokuwa hatarini."

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres aliitaja hatua iliyochukuliwa na jeshi "pigo kubwa kwa mabadiliko ya kidemokrasia", huku baraza la usalama likijitayarisha kufanya mkutano wa dharura.

Umoja wa Mataifa imetaka kuachiliwa kwa watu wasiopungua 45 ambao wanazuiliwa na jeshi.

Nchini Uingereza, Waziri Mkuu Boris Johnson ameshutumu mapinduzi hayo na kuzuiliwa kwa Aung San Suu Kyi ambako ni "kinyume na sheria".

Viongozi wa Umoja wa Ulaya wametoa shutuma zao sawa na hizo.

China, ambayo awali ilipinga muingilio wa mashirika ya kimataifa kwa nchi ya Myanmar, ilitoa wito kwa pande zote mbili "kutatua tofauti zao".

Baadhi ya mataifa jirani yenye nguvu kama vile Cambodia, Thailand na Ufilipino, yamesema kwamba hilo ni "suala la ndani".



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...