Search This Blog

Friday, February 26, 2021

Jeshi la Myanmar lafutilia mbali matokeo ya uchaguzi wa 2020


Utawala wa jeshi ambao ulichukua madaraka kwa nji ya mapinduzi nchini Myanmar, ulifutilia mbali matokeo ya uchaguzi mkuu wa 2020, ambapo chama cha Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje na kiongozi wa nchi, Aung San Suu Kyi, kiliibuka wa kwanza.

Thein Soe ambaye ni Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Muungano ambayo ilianzishwa baada ya mapinduzi, alitangaza katika mkutano na wawakilishi wa vyama vya siasa kwamba matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 8 Novemba 2020 yalifutiliwa mbali kutokana na madai ya udanganyifu.

Kati ya vyama 93 vya kisiasa vilivyosajiliwa nchini humo, vyama 53 pekee ndivyo vilivyohudhuria mkutano huo.

Katika uchaguzi mkuu wa Novemba 2020, chama cha NLD kinachoongozwa na Aung San Suu Kyi, kilidumisha nguvu yake kwa kushinda viti 238 katika bunge na viti 138 katika seneti.

Katika shughuli ya kuhesabu kura, ilidaiwa kuwa maafisa wa NLD walitekeleza udanganyifu kwa kuhesabu kura za chama mara mbili au tatu katika masanduku mengi ya kura.

Licha ya madai hayo, tume ya uchaguzi iliamua kupuuzia mbali kwa kusema hayana msingi na kwamba NLD ilishinda uchaguzi.

Wakati vyama vinavyounga mkono jeshi na wapinzani wamekuwa wakipinga matokeo ya uchaguzi tangu mwanzoni mwa mwaka, Mkuu wa Idara ya Wafanyikazi wa Umma Min Aung Hlaing, alitangaza mnamo Januari 27 kwamba katiba inaweza kufutwa ikiwa serikali haichukui hatua juu ya madai ya udanganyifu ya uchaguzi.

Jeshi la Myanmar lilipindua serikali ya utawala mnamo Februari 1, baada ya vyama vya kisiasa vilivyo karibu nao kutoa madai ya udanganyifu katika uchaguzi.

Jeshi lilitangaza hali ya hatari kwa mwaka mmoja na kukamata maafisa wengi na viongozi wa chama tawala akiwemo Aung San Suu Kyi.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...