Search This Blog

Tuesday, February 16, 2021

Chanjo ya AstraZeneca kufanyiwa majaribio kwa watoto


Chuo Kikuu cha Oxford na kampuni ya dawa ya AstraZeneca imetangaza kuwa itafanya majaribio ya chanjo waliyotengeneza dhidi ya corona (Covid-19) kwa watoto wenye umri wa kati ya miaka 6-17.

Kulingana na habari ya BBC, usajili wa kujitolea wa majaribio ya kliniki umeanza kufanywa katika Hospitali ya Chuo Kikuu cha Oxford St George, Hospitali ya Chuo Kikuu cha Southampton na Hospitali ya watoto ya Bristol Royal.

Katika majaribio hayo ambapo watoto 300 wamepangwa kushirikishwa, chanjo ya Covid-19 itapewa watoto 240 katika kikundi cha majaribio, na chanjo udhibiti itapewa kwa watoto 60.

Majaribio yanalenga kupima athari za chanjo katika kuzuia maambukizo kwa watoto.

Majaribio ya kliniki ya chanjo ya Oxford-Zeneca hapo awali yalifanywa kwa watu wenye umri wa kati ya miaka 18-64 na zaidi ya 65.

Kampuni ya kibayoteki ya Ujerumani ya BioNTech na kampuni ya dawa ya Marekani ya Pfizer pamoja na kampuni ya kibayoteki ya Marekani ya Moderna pia zilitangaza kuwa zitafanya majaribio ya chanjo ya Covid-19 ambazo wameandaa kwa watoto wenye umri wa kati ya miaka 12-17.

Hadi sasa bado hakuna chanjo ya Covid-19 iliyoidhinishwa kutumiwa kwa watoto ulimwenguni. Ni chanjo ya BioNTech-Pfizer tu ambayo inaweza kutolewa kwa watoto wa miaka 16 chini ya matumizi ya dharura nchini Marekani.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...