Search This Blog

Sunday, February 14, 2021

Balozi wa Israel Marekani asema Netanyahu hana wasiwasi kutopigiwa simu na Biden

 


Balozi wa Israel nchini Marekani Gilad Erdan, amesema jana kuwa waziri wake mkuu Benjamin Netanyahu hana wasiwasi wowote kwamba rais wa Marekani Joe Biden hajampigia simu huku akionekana kujaribu kupuuza ukosefu huo wa mawasiliano ya moja kwa moja kufikia sasa. 


Erdan amesema kuwa Netanyahu hana wasiwasi kuhusu wakati wa mazungumzo na kwamba Biden ana masuala muhimu ya kushughulikia kama vile janga la virusi vya corona na kudorora kwa uchumi. 


Siku ya Ijumaa ikulu ya White House ilikanusha kwamba Biden alikuwa anampuuza Netanyahu kimaksudi kwa kukosa kumjumuisha katika mawasiliano ya simu na viongozi wa kigeni kufikia sasa tangu alipochukuwa hatamu za uongozi mnamo Januari 20 na kusema viongozi hao wawili watazungumza karibuni. 


Kumekuwa na uvumi kwamba Biden anaonyesha ishara ya kutoridhishwa na uhusiano wa karibu aliokuwa nao Netanyahu na rais wa zamani Donald Trump, aliyempigia simu siku mbili baada ya kuapishwa kwake mnamo mwaka 2017.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...