Search This Blog

Sunday, February 14, 2021

Anjella apelekwa mjini kwa Kiingereza

 


Msanii wa Bongofleva Harmonize, amesherehekea siku ya Valentine kwa kuachia ngoma yake mpya #AllNight aliyomshirikisha msanii chipukizi Anjella.


Harmonize ametimiza ahadi yake kwa Anjella kuwa atampeleka mjini, mara tu baada ya kuona clip zake akiimba na kuvutiwa na kipaji chake.


Katika ngoma hiyo Anjella ameimba chorus na lugha iliyotumika kwa kiasi kikubwa ni Kiingereza. Kwa mujibu wa Harmonize, hii ndio single yake ya kwanza official kuitoa kwa mwaka 2021.


Harmonize ameanza na audio na huenda akaachia video ya ngoma hiyo muda si mrefu, kwani tayari alishadokeza kuwa ipo tayari muda mrefu.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...