Mahakama ya kikatiba ya Afrika Kusini imesema kuwa rais wa zamani Jacob Zuma ni lazima afike mbele ya jopo linalochunguza madai ya vitendo vya rushwa vilivyotokea wakati wa utawala wake.
Mahakama iliamua kuwa kuwa hakuwa na haki kukaa kimya mbele ya tume.
Bwana Zuma anashutumiwa kupora mali za taifa hilo wakati alipokuwa rais.
Zuma amekana madai hayo dhidi yake.
Matokeo ya jopo hilo hayatawaongoza moja kwa moja kwenye mashtaka lakini yanaweza kupelekwa kwa waendesha mashtaka.

No comments:
Post a Comment