Search This Blog

Tuesday, January 5, 2021

ZSSF yaagizwa kusimamia amana za Wanachama


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Mwinyi amesema kuwa, Serikali itaendelea kushirikiana na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) ili kuhakikisha amana zote za Wananchama zinasimamiwa ipasavyo.

Dkt Mwinyi ametoa kauli hiyo wakati wa ufunguzi wa jengo jipya linalojulikana kama Hifadhi Building, linalomilikiwa na ZSSF lililoko Tibirinzi wilaya ya Chake Chake mkoa wa Kusini Pemba.

Amesema ni jukumu la Serikali kuhakikisha inachukua hatua zinazofaa na kwa wakati, kuhakikisha ZSSF inaendelea kuimarika, inaongozwa na kusimamiwa na Viongozi walio makini na wanaojiepusha na vitendo vya ubadhirifu, rushwa na wizi.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...