Search This Blog

Tuesday, January 26, 2021

Wawili yanga wapo chini ya Uangalizi


 UONGOZI wa Yanga umesema kuwa nyota wao wawili bado wapo kwenye uangalizi wa jopo la madaktari kabla ya kurejea uwanjani.

Kwa sasa kikosi hicho ambacho kinanolewa na Kocha Mkuu, Cedric Kaze kimeshawasili kambini na kilianza mazoezi rasmi Januari 25,Kigamboni.

Akizungumza na Saleh Jembe, Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh amesema kuwa maendeleo ya wachezaji wao wawili ambao ni Saido Ntibanzokiza na Yacouba Songne ni mazuri.

"Wachezaji wetu wote ambao wameshawasili kambini wanaendelea vizuri na tayari mazoezi yanaendelea ambapo ni Saido na Yacouba hawa bado hawajawa kwenye ubora wao.

"Wapo kwenye uangalizi wa jopo la madaktari na tunaamini kwamba watakuwa imara na watarejea uwanjani,".

Yanga ipo nafasi ya kwanza ikiwa na pointi 44 baada ya kucheza jumla ya mechi 18.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...