Search This Blog

Sunday, January 17, 2021

Vikosi vya Umoja wa Mataifa CAR vyaurejesha mji uliodhibitiwa na waasi

 


Vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati vimedai kurejesha udhibiti wa mji ambao awali ulikamatwa na waasi katikati ya taifa hilo. 

Mji huo ulichukuliwa na waasi ambao walijihami kwa silaha mapema mwezi huu. Waasi hao wanaipinga serikali ya rais Faustin Touadera. 

Msemaji wa serikali ya Touadera Vladimir Monteiro amesema mji wa Bangassou uko chini ya udhibiti kamili wa MINUSCA na kuongeza kuwa waasi waliutelekeza mji huo baada ya kupewa muda na vikosi hivyo siku ya Ijumaa.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...