Search This Blog

Sunday, January 31, 2021

Uingereza yaanzisha pasi mpya ya kusafiria kwa raia wa Hong Kong

 


Hatimaye raia wa Hong Kong sasa wanaweza kuomba uraia nchini Uingereza kuanzia hii leo baada ya visa mpya zinazotolewa na nchi hiyo kuwapatia fursa ya kuwa raia, kufuatia Beijing kuanzisha sheria mpya ya usalama wa taifa katika jiji hilo kitovu cha biashara barani Asia mwaka jana. 


Hatua hii inachukuliwa wakati China na Hong Kong zikiwa zimesema hazitaitambua tena pasi ya kusafiria ya Uingereza, kama hati halali ya kusafiria kuanzia leo. 


Uingereza inakisia kwamba kupitia viza hiyo huenda watu 300,000 pamoja na jamaa zao wataingia nchini humo. 


Uingereza na China zimekuwa zikizozana kwa miezi kadhaa juu ya sheria hiyo ambayo London na Washington zinasema ni hatua inayolenga kubana uhuru wa kujieleza kwa wakosoaji jijini Hong Kong baada ya maandamano ya wanaounga mkono demokrasia yaliyofanyika kati ya mwaka 2019 na mwaka jana.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...