Search This Blog

Friday, January 15, 2021

Tume ya Uchaguzi Uganda kupeperusha matokeo licha ya kufungwa kwa intaneti


Tume ya Uchaguzi nchini Uganda siku ya Alhamisi ilihakikisha kwamba matokeo ya moja kwa moja ya Uchaguzi katika kituo kikuu cha kujumlisha kura cha kitaifa yatendelea licha ya kufungwa kwa intaneti nchini humo.

Mkuu wa Tume ya Uchguzi Simon Byabakama alisema kwamba wanatumia mbinu fulani kurusha matokeo hayo lakini haikutoa maelezo zaidi.

‘’ Hatutumii intaneti ya nchini kurusha matangazo . Tunatumia mfumo wetu . Musijali, matokeo yatapeperushwa licha ya kwamba mtandao umefungwa’’ , aliambia waandishi.

Ilitoa matokeo ya awali siku ya Ijumaa kutoka vituo 330 ambayo yalimuonesha rais Yoweri Museveni akichukua uongozi wa mapema kulingana na gazeti la Daily Monitor.

Taifa hilo lina jumla ya vituo vya kupigia kura 34,684

Sheria ya Uganda inaipatia uwezo Tume hiyo kupokea matokeo kutoka wilaya zote na kuyatangaza katika muda was saa 48 baada ya shughuli ya kupiga kura kukamilika.





No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...