Search This Blog

Saturday, January 16, 2021

TANZIA: Msanii wa Bongofleva C Pwaa afariki Dunia

 


Msanii wa Bongofleva Ilunga Khalifa maarufu C Pwaa amefariki Dunia Alfajiri ya leo akiwa anapatiwa matibabu Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Kwa mujibu wa Ndugu wa karibu wa C Pwaa amethibitisha kuwa Pwaa alikuwa anaugua Pneumonia na alifikishwa Hospitali kwa matibabu, hali yake haikuwa njema hadi umauti unamkuta.

Enzi za uhai wake C Pwaa alifanya vizuri akiwa na kundi la Park Lane pamoja na Suma Lee ambapo walitoa ngoma kama Nafasi Nyingine na Aisha, na baadaye alitoa ngoma zake nje ya kundi zikiwemo Action, Problem, So Pwaa, Six in the Morning nk.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...