Search This Blog

Saturday, January 23, 2021

Shambulizi la kombora Iraq

Shambulizi la kombora lilitekelezwa kwenye Uwanja wa ndege wa Baghdad nchini Iraq.

Katika taarifa iliyotolewa na Wizara ya Ulinzi, iliripotiwa kuwa makombora matatu yalirushwa kwenye Uwanja wa ndege wa Baghdad katika shambulizi lililotokea usiku, ingawa hakuna watu waliouawa au kujeruhiwa.

Ilibainika kuwa makombora mawili kati ya yaliyorushwa yalianguka karibu na uwanja wa ndege, na kombora la tatu liligonga nyumba ya raia katika kitongoji cha Al-Jihad magharibi mwa Baghdad na kusababisha uharibifu.

Hakuna mtu aliyedai kuhusika na shambulizi hilo.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...