Shambulizi la kombora lilitekelezwa kwenye Uwanja wa ndege wa Baghdad nchini Iraq.
Katika taarifa iliyotolewa na Wizara ya Ulinzi, iliripotiwa kuwa makombora matatu yalirushwa kwenye Uwanja wa ndege wa Baghdad katika shambulizi lililotokea usiku, ingawa hakuna watu waliouawa au kujeruhiwa.
Ilibainika kuwa makombora mawili kati ya yaliyorushwa yalianguka karibu na uwanja wa ndege, na kombora la tatu liligonga nyumba ya raia katika kitongoji cha Al-Jihad magharibi mwa Baghdad na kusababisha uharibifu.
Hakuna mtu aliyedai kuhusika na shambulizi hilo.

No comments:
Post a Comment