Search This Blog

Wednesday, January 27, 2021

Rais Magufuli kuzindua shamba la miti lililopo Butengo, Chato


 Leo Januari 27, 2021, Rais Magufuli atazindua shamba la miti lililopo Butengo, Chato Geita, shamba ambalo linaelezwa kuwa mpaka sasa limeshatoa ajira mbalimbali kwa wakazi wa eneo hilo hali iliyopelekea kuongeza uchumi wa mtu mmoja mmoja.

Shamba la miti la Chato lenye ukubwa wa hekta 69,000, lilianzishwa mwaka 2017 baada ya uharibifu mkubwa uliofanywa na wanachi kuvamia shamba hilo na ndipo serikali kupitia wakala wa misitu (TFS), wakaamua kuendeleza shamba hilo ili kutunza mazingira.

Imeelezwa kuwa shamba hilo ni la pili kwa ukubwa kati ya mashamba yanayomilikiwa na Serikali na limeanzishwa kama sehemu ya eneo la msitu mkubwa wa Hifadhi ya Biharamulo-Alabama, ni la pili kwa ukubwa baada ya Saohill.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...