Ndege 750 wameripotiwa kuangamia katika mbuga ya hifadhi ya kaskazini mwa Senegal kutokana na homa ya ndege.
Waziri wa Mazingira Abdou Karim Sall , alitangaza kwenye kituo cha redio cha Rfm kuwa ndege 750 waliangaia kutokana na homa ya ndege mnamo Januari 23, katika hifadhi ya ndege ya Djoudj iliyoko eneo la Saint-Louis.
Sall alisema kuwa hifadhi hiyo ilifungwa kwa wageni na kutoa onya kwamba ugonjwa huo unaweza kuenea haraka sana kutokana na msimu wa uhamiaji.
Hifadhi ya ndege ya Djoudj, ambayo iko kwenye Orodha ya Urithi wa Dunia wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), inatoa hifadhi kwa aina 400 za ndege katika eneo la ukubwa wa hekta elfu 16.
Katika hifadhi hiyo, ndege 750 waliangamia mnamo Januari 23, kwa sababu isiyojulikana na mizoga yao ilipelekwa kufanyiwa uchunguzi.

No comments:
Post a Comment