Mazungumzo juu ya kuunda katiba mpya ya Syria yamegonga mwamba na mpatanishi wa Umoja wa Mataifa amesema mambo hayawezi kuendelea katika njia hiyo.
Wawakilishi kutoka serikali ya rais Bashar al Assad,wapinzani na asasi za kiraia waliokutana mjini Geneva kwa muda wa wiki nzima walimaliza mazungumzo bila ya mafanikio.
Mpatanishi wa Umoja wa Mataifa Geir Pedersen amekiri kwamba hakuna kilichofikiwa.Bwana Pedersen amesema mapendekezo yaliyotolewa na wapinzani juu ya kuyasogeza mbele mazungumzo yalikataliwa na wajumbe wa serikali ya Assad.
Mwaka uliopita kamati maalumu juu ya katiba ya Syria iliundwa kwa lengo la kuutatua mgogoro wa nchi hiyo na hivyo kuvimaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyozuka mnamo mwaka 2011.
Watu wapatao 390,000 wameshakufa kutokana na vita hivyo.

No comments:
Post a Comment