Search This Blog

Friday, January 1, 2021

Makao makuu ya Haftar yavamiwa Libya


Waandamanaji wa Libya wamevamia makao makuu ya eneo la Hun katika mji wa al-Jufra, yanayohusiana na vikosi haramu vya wanajeshi wa Khalifa Haftar.

Katika taarifa iliyoandikwa na Ofisi ya Mawasiliano ya Operesheni ya Volkano inayoendeshwa na jeshi la Libya, iliarifiwa kwamba wanaharakati waliojibu mashambulizi endelevu ya dhidi ya raia katika mji wa al-Jufra, walivamia vikosi hivyo na kudai wanajeshi wa kulipwa wakabidhiwe kwao.

Wakazi wa eneo la Hun walipinga mauaji ya vijana wawili na wanamgambo wa Janjaweed yaliyotokea mnamo Julai 11. Katika mwezi huo huo, mtu mwingine pia aliuawa na wanamgambo wa Janjaweed mbele ya nyumba yake.

Nchi ya Falme za Kiarabu (UAE) ambayo ni msaidizi mkubwa wa kifedha, kisiasa na kijeshi wa Haftar, alituma maelfu ya wanajeshi wa kulipwa waliofungamana na kampuni ya usalama ya Urusi ya Wagner, pamoja na wapiganaji wa Syria na wanamgambo wa Janjaweed wa Sudan ili kusaidia kupigana katika safu ya Haftar.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...