Mahakama nchini Urusi hii leo imeagiza kiongozi wa upinzani Alexei Navalny kuendelea kushikiliwa kizuizini hadi Februari 15, katika kikao cha kusikiliza madai dhidi yake kilichopangwa kwa dharura baada ya kukamatwa kwake. Wakili wa Navalny Vadim Kobzev aliandika kwenye ukurasa wake wa twitter kutokea kwenye chumba cha mahakama kilichojengwa kwa muda kwenye kituo cha polisi kwamba mahakama imeamua Navalny kuendelea kushikiliwa kwa siku 30 kuanzia siku ya Jumapili alipokamatwa. Awali, waziri wa mambo ya kigeni wa Urusi Sergei Lavrov alisema Urusi haina uthibitisho wa madai yanayotolewa na mataifa ya magharibi kwamba kiongozi huyo wa upinzani alipewa sumu, zaidi ya ushahidi uliotolewa na yeye mwenyewe. Navalny alikamatwa jana alipokuwa anarejea kutoka Ujerumani alikokuwa akitibiwa kufuatia shambulizi la sumu, na kuituhumu Ikulu ya Kremlin kwa shambulizi hilo.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment