Search This Blog

Sunday, January 24, 2021

Jiwe la mwezini kupamba ofisi ya Biden


Rais Joe Biden ambaye alichukuwa wadhifa wa urais kutoka kwa Donald Trump nchini Marekani, anaendelea na shughuli za mabadiliko katika Ikulu ya White House.

Biden hivi karibuni aliweka jiwe la mwezini katika Oval Office, ambalo lililetwa Duniani kwa msafara wa Apollo 17 mnamo 1972.

Ilitangazwa kuwa jiwe lenye uzani wa gramu 333 lilikopwa kutoka Kituo cha Kitaifa cha Anga na Utawala wa Anga (NASA) cha Johson Space huko Houston.

Kulingana na taarifa za Washington Post, Rais Biden aliweka Jiwe la Mwezini katika Oval Office kama ukumbusho wa uvumilivu na mafanikio ya vizazi vilivyopita.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...