Search This Blog

Monday, January 4, 2021

Hamis wa BSS amuangukia Harmonize "Naomba anisamehe"


Ni 'headlines' za Hamis wa BSS msanii aliyejipatia umaarufu kupitia mashindano ya kusaka vipaji Bongo, ameonekana kumwaga machozi kwa boss wa lebo ya Konde Gang Harmonize huku akitaka msaada kutoka kwa msanii huyo.

Hamis Bss amefika mbali zaidi kwa kusema kama msanii huyo amemkosea basi anaomba amsamehe kwani mwanzo alionesha nia ya kutaka kumsapoti wakati alipokuwa kwenye mashindano.

"Ningeomba sana anisaidie, ujue mpaka mtu anafikia hatua ya kulia kwa ajili ya kuomba msaada sio poa, anisadie kwa chochote kile hata kwa wimbo mmoja au video tu kwa sababu anajuana na watu wengi, alivyosemaga kwamba atanisaini na kunisaidia nilidhani nimeshatoboa au kama nimemkosea naomba anisamehe" ameeleza Hamis



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...