Rais wa zamani wa Tunisia Moncef Marzouki amesema kuwa Rais Recep Tayyip Erdoğan daima ameunga mkono hoja ya Mohamed Morsi, Rais wa kwanza aliyechaguliwa kidemokrasia nchini Misri.
Katika hafla ya maadhimisho ya miaka 10 ya Mapinduzi ya Januari 25, Morsi Democracy Foundation iliandaa hafla na kaulimbiu "Miaka 10 Tangu Januari ... Morsi katika Moyo wa Mapinduzi" kupitia njia ya mkutano wa video.
Moncef Marzouki, mmoja wa washiriki wa hafla hiyo, alisema kuwa Morsi alikuwa akihangaika kuanzisha tena msimamo wa Misri katika ulimwengu wa Kiarabu na kuifanya nchi hiyo kuwa sheria.
Akizungumzia saada wa Rais Erdoğan kwa Morsi, Marzouki alisema,
"Rais Recep Tayyip Erdoğan aliunga mkono hoja ya Morsi nchini mwake na kimataifa."
"Morsi alijitahidi kwa maadili ya kibinadamu bila kuogopa matokeo yake, na licha ya kupingwa, alifuata demokrasia. Alikuwa mtu kamili kwa kila hali.", aliongeza kiongozi huyo.
Miaka 30 ya utawala wa Hosni Mubarak huko Misri ilimalizika na ghasia zilizoanza Januari 25, 2011. Mohammed Morsi, mmoja wa watu wa mfano wa Mapinduzi ya Januari 25 na Rais aliyechaguliwa kidemokrasia, aliondolewa katika wadhifa wake katika mapinduzi ya kijeshi mnamo Julai 2013.
Morsi alipoteza maisha katika chumba cha mahakama mnamo Juni 17, 2019.

No comments:
Post a Comment