Search This Blog

Sunday, January 24, 2021

Boris Johnson asema yuko tayari kufanya kazi na Joe Biden

 


Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson amesema yuko tayari kufanya kazi na rais mpya wa Marekani Joe Biden katika malengo yao ya pamoja ikiwemo kushughulikia masuala ya mabadiliko ya tabia nchi. 

Waziri Mkuu Johnson ameyasema hayo hapo jana baada ya kuzungumza na Biden kwa njia ya simu. Amekaribisha pia hatua ya Marekani kujiunga tena na makubaliano ya Paris ya kupambana na mabadiliko ya tabia nchi. 

Kulingana na msemaji wa Boris Johnson, Ili kuendelea kuimarisha ushirikiano wa kihistoria kati ya Uingereza na Marekani juu ya masuala ya usalama na ulinzi, viongozi hao wawili wamejitolea kuendelea kuukumbatia muungano wa NATO na kuendeleza maadili ya pamoja katika kuunga mkono haki za binaadamu na kulinda demokrasia.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...