Search This Blog

Monday, January 25, 2021

Australia yaongeza uwezo wake wa jeshi la majini


Waziri wa Ulinzi wa Australia Linda Reynolds ametangaza kwamba wameamua kuongeza uwezo wa jeshi la majini, pamoja na makombora ya masafa marefu na torpedoes.

Linda Reynolds ametangaza kwamba takriban dola bilioni 1 zitawekezwa katika mfumo wa kuboresha na kuimarisha jeshi la majini.

Akisisitiza kuwa uwekezaji mpya utafanywa katika manowari na meli za mapambano Reynolds, aliongeza kwa kusema,

"Uwezo huu mpya utahakikisha  utulivu na usalama katika mkoa,".

Reynolds amebaini kuwa makombora ya masafa marefu ya kupambana na meli, torpedoes zitaimarisha ulinzi baharini pamoja na majini.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...