Waziri wa Ulinzi wa Australia Linda Reynolds ametangaza kwamba wameamua kuongeza uwezo wa jeshi la majini, pamoja na makombora ya masafa marefu na torpedoes.
Linda Reynolds ametangaza kwamba takriban dola bilioni 1 zitawekezwa katika mfumo wa kuboresha na kuimarisha jeshi la majini.
Akisisitiza kuwa uwekezaji mpya utafanywa katika manowari na meli za mapambano Reynolds, aliongeza kwa kusema,
"Uwezo huu mpya utahakikisha utulivu na usalama katika mkoa,".
Reynolds amebaini kuwa makombora ya masafa marefu ya kupambana na meli, torpedoes zitaimarisha ulinzi baharini pamoja na majini.

No comments:
Post a Comment