Search This Blog

Thursday, January 28, 2021

Afrika Kusini inatarajia dozi za chanjo wiki ijayo


Afrika Kusini Jumatatu itapokea dozi milioni moja ya chanjo ya Covid-19 kutoka India wakati inapambana na virusi vipya.

Waziri wa Afya Zweli Mkhize alisema dozi za AstraZeneca zitapitia michakato ya kitaalamu wakati wa kuwasili, ikiwemo kuhakikisha ubora wake.

"Michakato hii itachukua siku zisizopungua 10 na si chini ya siku 14 kukamilisha, ambapo tutakuwa tayari kusambaza chanjo hizo kwenye majimbo yote," alisema.

Serikali ilinunua dozi ya chanjo milioni 1.5 kwa Januari na Februari, na dozi za ziada milioni 20 zinatarajiwa mwezi Juni. Afrika Kusini ndio nchi iliyoathirika zaidi na janga la corona barani Afrika.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...