Search This Blog

Tuesday, December 15, 2020

Waziri wa Malawi aidhinisha Nabii Bushiri na mkewe warudishwe Afrika Kusini

 


Waziri wa usalama wa ndani ya nchi wa nchini Malawi , Richard Banda, amesaini nyaraka kwa ajili ya mchungaji tajiri na maarufu Shepherd na mke wake, Mary, vimeripoti vyambo vya habari vya Malawi.


Hii inafuatia ombi la mahakama ya nchi jirani ya Afrika Kusini ambako Bushiri na mke wake Mary wanasakwa na mashitaka ya utakasaji wa fedha na ufisadi.


Mahakama ya juu zaidi nchini Malawi iko tayari kuamua kuhusu kukamatwa kwa wawili hao baada ya kuachiliwa huru bila masharti na mahakama ya hakimu mkazi ambayo ilisema kuwa ilichukua uamuzi huo kwasababu hapakuwa na ombi rasmi la kumrejesha lililotolewa na Afrika Kusini.


Mahakama itaamua kuhusu kesi hiyo tarehe 22 Disemba, kwa mujibu wa gazeti la Daily Times newspaper.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...