Search This Blog

Thursday, December 10, 2020

Waziri Mkuu wa Msumbiji akataa kuwapa silaha raia kupambana na wanamgambo

 


Waziri Mkuu wa Msumbiji, Carlos do Agostinho, amepinga wito wa kuwapa raia silaha katika jimbo la Cabo Delgado ili kupambana na wanamgambo wa Kiislamu.


Wakazi wa eneo hilo wakati wote wamekuwa wakiomba silaha ili kuvisaidia vikosi vya usalama.


Waziri Mkuu ametupilia mbali mawazo hayo wakati wa kikao cha masuala ya usalama kilichofanyika mji mkuu, Pemba.


Alisema kuwa hatua hiyo itakuwa ‘’hatari na isiyohimilika’’.


Alisisitiza silaha zinapaswa kuwa katika mikono ya ‘’watu wanaofaa’’, akimaanisha vikosi vya ulinzi na usalama na wale wanaowaamini.


Bwana do Rosario amesema raia wanapaswa kuwa na jembe la kulima na ardhi na kalamu ya kuchangia maendeleo ya taifa lao.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...