WAZIRI wa mifugo na Uvuvi Mh. Mashimba Mashauri ameahidi kuingilia kati kwa kulivalia njugaS Sakata la kunyimwa vibali kwa ajili ya kuuza nyama katika nchi ya nje kwa lengo la kuweza kuwaondolea wawekezaji changamoto hiyo ambayo inawakabili na kupelekea kukwamisha malengo waliyojiwekea katika kukuza uchumi wa nchi kupitia sekta ya viwanda.
Kwa upande wake Kaimu Msajili wa Bodi ya Nyama Tanzania (TMB) Imani Sichalwe amesema kwamba kwa sasa wameshaanza mipango ya kuzungumza na baadhi ya mabalozi wa nchi husika hususan za Uharabuni ili kuona namna ya kuweza kupata vibali na kuwasaidia wafugaji waweze kupata soka la uhakika.
Naye Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijiji Michael Mwakamo amebainisha kuwa ujenzi wa kiwanda hicho utakuwa ni mkombozi mkubwa katika suala zima la kukuza uchumi pamoja na kuwapatia vijana fursa za ajira na kuondokana na wimbi la umasikini.

No comments:
Post a Comment