Warembo 20 wanaowania taji la Miss Tanzania 2020 wamemtembelea Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Abubakar Kunenge, kwake.
Warembo hao kutoka kanda tofauti nchini, leo Jumamosi watapanda jukwaani kuwania taji la mwaka huu.
Fainali hiyo itafanyika kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere, Jijini Dar es Salaam (JNICC) ambapo mshindi atazawadiwa gari aina ya Subaru Impreza wakati mshindi wa pili atapewa kiwanja eneo la Kigamboni.
No comments:
Post a Comment