Search This Blog

Sunday, December 6, 2020

Wananchi wa Kuwait waanza zoezi la upigaji kura kwenye uchaguzi wa bunge


Nchi ya Kuwait imeandaa uchaguzi wa bunge katika kipindi cha janga la corona  (Covid-19).

Zoezi la upigaji kura lilianza nyakati za asubuhi ili kubainisha wabunge 50 watakaochaguliwa kuwakilisha bunge la taifa la Kuwait. 

Katika uchaguzi huo ulioandaliwa kwa kuzingatia tahadhari za janga la corona, jumla ya wagombea 326 wakiwemo wanawake 28 wanashindana. 

Nchi hiyo imegawanywa katika maeneo bunge 5 ambapo jumla ya watu 567,694 walisajiliwa kama wapiga kura. 

Wapigaji kura watachagua wagombea kumi kutoka kila eneo bunge watakaowawakilisha bungeni.

Zoezi la upigaji kura lilitatarajiwa kuendelea mpaka saa 20:00.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...