Search This Blog

Thursday, December 31, 2020

Vanessa Mdee avalishwa pete ya uchumba na Rotimi


Staa wa Tanzania aliyetangaza kuacha muziki Vanessa Mdee, amevalishwa pete ya uchumba na mpenzi wake Rotimi ambaye ni msanii wa filamu na mwanamuziki Rotimi ambao wanaishi wote kwa sasa nchini Marekani.

Kupitia 'videos clip' ambazo zimepostiwa kwenye mitandao ya kijamii zimeonyesha Rotimi akiwa amepiga magoti mbele ya Vanessa Mdee huku akimvalisha pete hiyo ya uchumba, kisha wakakumbatiana na kuanza ku-kiss.

Ikumbukwe tu mwanzoni mwa mwezi wa kumi mwaka 2020, Vanessa Mdee na Rotimi walishea picha mitandaoni zikiwaonyesha wamechorana 'tattoo' zenye majina yao kwenye miili yao.

Penzi la wawili hao lilianza Oktoba 2019, baada ya Vanessa Mdee kuachana na mkali wa RnB Bongo Juma Jux ambao walidumu kwa miaka 6.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...