Search This Blog

Tuesday, December 29, 2020

Ukraine yajiondoa kwenye mkataba wa mawasiliano kati ya serikali


Ukraine imejiondoa kutoka "mkataba wa mawasiliano kati ya serikali" na Jumuiya ya Madola ya Mataifa Huru.

Mwakilishi wa serikali ya Ukraine Vasiliy Mokan, alitoa taarifa kuhusu mkataba wa mawasiliano kati ya serikali husika.

Kwa kuzingatia uchokozi wa Urusi, Mokan alielezea kuwa utekelezaji wa mkataba wa mawasiliano na Ukraine unakuwa ni tishio kwa masilahi ya kitaifa ya nchi hiyo.

Vasiliy Mokan alifahamisha kuwa Baraza la Mawaziri lilipitisha "sheria ya kujiondoa kwenye makubaliano yanayohusu itifaki katika sekta ya mawasiliano kati ya serikali."

Mnamo Desemba 16, Ukraine ilitangaza kujiondoa kutoka kwa mfululizo wa mikataba na Jumuiya ya Madola ya Mataifa Huru katika sekta ya nishati.




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...