Ukraine imejiondoa kutoka "mkataba wa mawasiliano kati ya serikali" na Jumuiya ya Madola ya Mataifa Huru.
Mwakilishi wa serikali ya Ukraine Vasiliy Mokan, alitoa taarifa kuhusu mkataba wa mawasiliano kati ya serikali husika.
Kwa kuzingatia uchokozi wa Urusi, Mokan alielezea kuwa utekelezaji wa mkataba wa mawasiliano na Ukraine unakuwa ni tishio kwa masilahi ya kitaifa ya nchi hiyo.
Vasiliy Mokan alifahamisha kuwa Baraza la Mawaziri lilipitisha "sheria ya kujiondoa kwenye makubaliano yanayohusu itifaki katika sekta ya mawasiliano kati ya serikali."
Mnamo Desemba 16, Ukraine ilitangaza kujiondoa kutoka kwa mfululizo wa mikataba na Jumuiya ya Madola ya Mataifa Huru katika sekta ya nishati.

No comments:
Post a Comment