Kiongozi wa chama cha upinzani nchini Tanzania, Chadema,bwana Tundu Lissu ametunukiwa tuzo ya demokrasia.
Taasisi ya kimataifa ya 'International Democrat Union' imemtunuku tuzo hiyo kutokana na mapambano yake ya uhuru na demokrasia aliyoyafanya nchini Tanzania.
Mara baada ya matokeo ya uchaguzi uliofanyika mwezi Oktoba kutangazwa, Lissu alisema kuwa alikuwa akipokea vitisho vya kifo hatua iliomfanya kuondoka na kuelekea Ubelgiji.

No comments:
Post a Comment