Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) kupitia Wizara ya Sayansi na Teknolojia imetoa shilingi milioni 120/- kwa ajili ya kuendesha mafunzo ya wajasiliamali 422 wilayani Sengerema katika Mkoa wa Mwanza
Fedha hizo zimepitia chuo Cha maendeleo ya Wananchi Sengerema (FDC) ambao ndiyo wanatoa mafunzo hayo kwa wajasiliamali hao yanatolewa bure.
Akisoma taarifa ya chuo hicho kwenye uzinduzi wa mafunzo hayo mkuu wa chuo Hagai Shilah alisema mafunzo hayo yanayotolewa yamefadhaliwa na Mamulaka ya Elimu Tanzania (TEA) kupitia mradi wa kukuza ujuzi na stadi za kazi (SDF) .
Kupitia mfumo wa kukuza ujuzi(Skills development funds) (SDF) fedha hizo hutolewa kwa awamu tatu ,ambazo ni awamu ya kwanza 40% awamu ya pili 40%na awamu ya tatu 20% kadri mradi utavyotekelezwa hadi sasa chuo kimepokea awamu mbili za fedha S48,000.
"Tunawaomba wanasengerema wajitokeze kupata mafunzo hayo kwa kuwa yanatolewa bure yatawasaidia kujifunza stadi za kazi na kuendesha maisha yao "alisema Shilah.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Sengerema Magesa Mafuru ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa mafunzo haya amewataka waliopata na wanaoendelea kupata mafunzo hayo kutumia ujuzi huo ili kuwaletea maendeleo kwenye maisha yao.
Sambamba na hayo amewataka washiriki wa mafunzo hayo kuunda vikundi ili kupata mikipo inayotolewa na Halmashauri ya Sengerema kwa vijana, akina mama na watu wenye ulemavu.
Elizabeth Matayo ambaye ni mlemavu wa ngozi ambaye anapata mafunzo ya Ushonaji kupitia maradi wa (TEA) alisema licha ya kuwa mlemavu wa ngozi mafunzo haya ya yatamsadia kuendesha maisha kwa kuwa sasa anajua kushona nguo.
Moja wa washikiriki wa mafunzo hayo Naoami Costantin alisema tangua wapate mafunzo haya wameelewa kushona , kudalizi na kushona masweta na kutoa wito kwa wanasichana kuacha tabia ya kufanya biashara ya ngono badara yake waje wapate ujuzi kupitia mafunzo haya na kijikimu kimaisha.

No comments:
Post a Comment