Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) wilaya ya Simanjiro imeadhimisha siku ya maadili kwa kusikiliza kero za wananchi vijijini mbalimbali wilayani hapo.
Mbele ya mkuu wa TAKUKURU wilaya ya Simanjiro Adam Kilongozi, Wananchi katika Kijiji cha Oiborkishu kilichopo kata ya Oljoro Na. 5 walitoa malalamiko yao walieleza kuwa wanachangishwa michango bila kupewa risiti.
Kilongozi aliwasisitiza wananchi hao kuendelea kutoa taarifa za vitendo vya Rushwa bila kutishwa na mtu yeyote.
No comments:
Post a Comment